• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

ZIARA YA MKUU WA MKOA PAMOJA NA KAMATI YA SIASA MKOA WA IRINGA KUKAGUA MIRADI KATIKA HARMASHAURI YA MANISPAA IRINGA

Posted on: January 19th, 2022

ZIARA YA MKUU WA MKOA PAMOJA NA KAMATI YA SIASA MKOA WA IRINGA KUKAGUA MIRADI KATIKA HARMASHAURI YA MANISPAA IRINGA.

WAKAZI wa kata ya Mkimbizi na maeneo jirani mjini Iringa wanatarajia kuanza kupata huduma za afya kupitia kituo cha Afya Mkimbizi, kinachojengwa katika kata hiyo kwa zaidi ya Sh Milioni 250.

Fedha hizo ni sehemu ya makusanyo ya tozo ya miamala ya simu zilizotolewa na serikali kwa halmashauri ya manispaa ya Iringa ili kuwezesha ujenzi wa kituo hicho katika kata hiyo yenye idadi kubwa ya watu, mjini Iringa.

Mbali na kituo hicho, serikali pia imetoa Sh Milioni 12.5 za tozo hizo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Sekondari Ipogolo.

Taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh.Queen Sendiga imepongeza ujenzi wa miradi hiyo iliyoelezwa kwamba itasaidia kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani.

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa ilitembelea miradi hiyo hivikaribuni na kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wake.

Wakati mradi wa ujenzi wa kituo cha afya umefikia asilimia 60, madarasa mawili katika shule ya sekondari Ipogolo yamekamilika na tayari yameanza kutumiwa na wanafunzi wa shule hiyo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Abel Nyamahanga alisema ujenzi wa majengo hayo (kituo cha afya na madarasa) utasaidia sana katika kuboresha huduma katika manispaa hiyo.

“Tunaanza kuona umuhimu wa tozo kila tunapoona miradi kama hii. Tuna kila sababu ya kuunga mkono mipango ya serikali kwani faida zake ni nyingi na muhimu kwa wananchi wote,” alisema.

Wakati huo huo kamati hiyo imeridhishwa pia na ujenzi wa barabara ya Don Bosco Mawelewele- Zizi na Kitasengwa inayojengwa kwa kiwango cha lami.

Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura) wa wilaya ya Iringa, Barnabas Jabiry alisema wakati barabara ya Donbosco Mawelewele ina urefu wa kilometa moja ya Kitasengwa ni ya kilometa 0.65.

Mbali na kupendezesha mji, Jabiry alisema miradi hiyo itakapokamilika itapunguza adha ya usafiri kwa wakazi wa kata ya Mwangata, Mkwawa na Isakalilo mjini Iringa.

“Kupitika vizuri kwa barabara hizo kutasababisha wananchi husika kuweza kufanya shughuli zao za kijamii na kiuchumi kwa urahisi,” alisema.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Iringa amesema ujenzi wa machinjio ya kisasa ya Ngelewala umefikia zaidi ya asilimia 90.

Mh.Sendiga amesema“matarajio ya mkoa na manispaa ya Iringa ni kuona kwamba machinjio hiyo inaanza kufanya kazi ifikapo Machi mwaka huu.”



Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.