• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WATU WENYE MAHITAJI MAALUMU KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU

Posted on: December 15th, 2024

Makamu Mwenyekiti tume huru ya Taifa ya uchaguzi, Jaji (R) (MST) Mbarouk S. Mbarouk amesema kuwa watu wenye mahitaji maalumu watapewa kipaumbele cha kujiandikisha bila ya kulazimika kusubiri kupanga foleni.

Mhe. Mbarouk ameyasema hayo  Disemba 15, 2024 Wakati akifungua  mkutano wa tume na Wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa uliyopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wenye kauli mbiu ya inayosema "Kujiandikishia kuwa mpiga kura ni msingi wa uchaguzi bora".

Akizungumza katika ufunguzi huo Mhe. Mbarouk amefafanua kwamba hatua hii inalenga kuhakikisha kuwa haki za watu wenye ulemavu, wazee, na makundi mengine yenye mahitaji maalumu zinaheshimiwa na kutekelezwa kwa usawa hivyo  mchakato wa kujiandikisha katika daftari la kudumu utaendelea kuwa rahisi kwa watu hao ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchaguzi bila vikwazo vya aina yoyote.

"Ni muhimu kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anapata fursa ya kushiriki katika uchaguzi bila kujali changamoto anazokutana nazo, Kwa hiyo watu wenye mahitaji maalumu watapewa kipaumbele maalumu katika vituo vya kujiandikisha ili wasiwekewe vikwazo vya aina yoyote na hakuna mtu atakayezuiliwa kutokana na hali yake ya kiafya au kimwili", amesema Mbarouk


Pia ameongeza kwa kusema  kuwa Tume ya Uchaguzi itahakikisha kuwa vituo vya kujiandikisha vitakuwa na mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu, ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa vifaa na msaada wa ziada ili kuwasaidia katika mchakato huo na kuongeza kwa kutoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano na kuhamasisha watu wenye mahitaji maalumu kujitokeza na kujiandikisha ili waweze kutumia haki yao ya kupiga kura katika uchaguzi ujao.


Mkutano huo uliofanyika Mkoani Iringa ni sehemu ya jitihada za Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kuelimisha na kuwashirikisha wadau wa uchaguzi kuhusu umuhimu wa kujiandikisha kama wapiga kura na umuhimu wa kuwa na daftari la mpiga kura.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC SERUKAMBA AMESHIRIKI NA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MAZISHI YA MDOGO WAKE NA WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU MHE WILLIAM LUKUVI

    June 07, 2025
  • WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA

    June 06, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA KITAIFA YATAFANYIKA MKOA WA IRINGA

    June 02, 2025
  • KAMBI YA MADAKTARI BINGWA YA MAMA SAMIA YATUA IRINGA

    June 02, 2025
  • Tazama zote

Video

WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.