• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WAFUJAJI FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO WANYOOSHEWA KIDOLE IRINGA

Posted on: September 12th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa- Iringa

Serikali ya Mkoa wa Iringa imewanyooshea kidole watumishi wanaogeuza fedha za miradi ya maendeleo kuwa sehemu ya kujinufaisha wenyewe tofauti na madhumini ya fedha hizo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi alipokuwa akiongea na wananchi wa Tarafa ya Sadani wilayani Mufindi leo katika siku yake ya nne ya ziara ya Tarafa kwa Tarafa wilayani Mufindi.

Mhe Hapi alisema “Serikali ya awamu ya tano inaleta fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi. Wapo baadhi ya watendaji wanazigeuza fedha za Serikali kama shamba la bibi. Nimekuja kuhakikisha tunasimamia vizuri miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha za Serikali. Leo nipo Tarafa ya nne tangu nimeanza ziara ya kutembelea Tarafa kwa Tarafa ambapo miradi mitatu nimeshawakabidhi TAKUKURU washughulike nayo kutokana na kutoridhika na jinsi fedha ya Serikali ilivyotumika” alisema Mhe Hapi.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa amekuja Iringa kuhakikisha miradi ya maji inatekelezwa vizuri na hakuna mchwa wanaotafuna fedha za Serikali katika miradi hiyo. “Tunafahamu kuwa yapo matatizo ya pembejeo kuchelewa, pembejeo kuuzwa kwa gharama kubwa kuliko bei elekezi za Serikali tunayatafutia ufumbuzi” alisema Mhe Hapi. Lengo la serikali ni kuona wakulima wananufaika na kilimo na kujiletea maendeleo, aliongeza.

Mkuu wa Mkoa aliwaasa watendaji wanaowanyanyasa wananchi. “Wapo baadhi ya watendaji ambao ni vinara wa kunyanyasa wananchi, mwenye pesa anapewa haki masikini ananyimwa haki. Kiongozi na mtendaji ambaye hatatui kero za wananchi hatufai. Hii ni nchi yetu sote, lazima tulinde rasilimali za nchi yetu na watu wake. Asiyeweza kwendana na kasi yangu aandike barua aache kazi akatafute kazi nyingine” alisema Mhe Hapi.

Akiwa katika Tarafa ya Sadani Mkuu wa Mkoa alikagua ujenzi wa tanki la maji kijiji cha Maduma, kukagua ufugaji wa nyuki, alikagua lambo la mifugo na shamba la matikiti maji la mwananchi. Shughuli nyingi alizofanya ni kukagua ujenzi wa hosteli ya sekondari Mgalo na kufanya mkutano na wananchi wa Tarafa ya Sadani na kusikiliza kero za wananchi.

=30=




Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.