• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

VIBALI ZIARA ZA KIELIMU KULINDA HAKI ZA WATOTO IRINGA-RC MASENZA

Posted on: June 7th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Serikali mkoani Iringa imetoa maelekezo kuwa vibali vyote vya ziara za elimu ziwe na mkakati wa kulinda haki za watoto dhidi ya ukatili wa aina yoyote.

Maelekezo hayo yalitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Mwl Amina Masenza katika hotuba yake kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya kusoma ngazi ya mkoa yaliyofanyika katika mji mdogo wa Ilula wilayani Kilolo.

Mwl Masenza aliitaka jamii nzima kuwa na sauti ya watoto kuripoti matukio yanayoashiria unyanyasaji wa watoto wote. “Ninaagiza vibali vyote vya ziara zote za kielimu zinazofanyika katika mkoa wetu ziwe na mkakati maalum wa kulinda haki za watoto na kuhakikisha hakuna ukatili wa aina yoyote unaofanyika kwa watoto wetu, kinyume na hapo kisitolewe kibali cha shughuli hizo” aliagiza Mwl Masenza. Vilevile, alizitaka shule zote zenye vyombo vya usafiri kuhakikisha wanapowarudisha watoto kunakuwa na usimamizi makini ili watoto wakubwa wasipate fursa ya kuwanyanyasa watoto wadogo katika vyombo vya usafiri.

Aidha, mkuu wa Mkoa aliwataka walimu kuzingatia nidhamu, uadilifu na uwajibikaji katika maeneo yao ya kazi. “Walimu mnawajibika kwa wanafunzi, kwa jamii kwenye kazi zenu, kwa mwajiri na taifa kwa ujumla. Wajibu wenu walimu ni kumlea mwanafunzi kiakili, kimwili na kiroho ili awe raia mwema na mzalendo wa nchi yetu” alisisitiza Mwl Masenza. Aliwataka walimu kujiepusha na ulevi, wizi, uasherati, rushwa na ubaguzi katika maeneo ya kazi.

Taarifa ya maadhimisho ya wiki ya kusoma Mkoa wa Iringa iliyowasilishwa na kaimu afisa elimu Mkoa wa Iringa, Mwl Farida Mwasumilwe alisema kuwa mpango wa kukuza stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) umepata mafanikio makubwa mkoani hapa. Alisema mpango huo umefanikiwa kuwapatia mafunzo ya stadi za KKK walimu 3,796 kati ya walimu 5326 sawa na asilimia 71.3. Mafanikio mengine aliyataja kuwa idadi ya wanafunzi wasiojua KKK imeshuka. Mkoa una wanafunzi 34,282 kati ya 38,562 wa darasa la pili wanajua kusoma sawa na asilimia 88.91, wanafunzi 4,279 hawamudu KKK. Uwepo wa vitabu vya ziada na kiada kwa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu, aliongeza Mwl Mwasumilwe. Mafanikio hayo yamechangiwa na juhudi za serikali za kukabiliana na changamoto za wanafunzi kutojua kusoma. Pia uwepo wa wa miradi mikubwa miliwi inayoendesha mafunzo ya KKK katika mkoa ambayo ni LANES na TUSOME PAMOJA.

Maadhimisho ya wili ya kusoma Mkoa wa Iringa yalitanguliwa na maadhimisho hayo katika ngazi za halmashauri kuanzia tarehe 31 Mei, 2018 hadi 6 Juni, 2018.

=30=


Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.