• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC – HAPI ASHAURI MITA ZA LUKU KWENYE MAJI

Posted on: September 20th, 2018

Na. Dennis Gondwe, Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-IRINGA

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Ally Hapi ameshauri mkoa wa Iringa kuangalia uwezekano wa kutumia huduma ya maji kwa njia ya luku ili kuepuka matumizi yasiyo ya lazima ya maji yanayopelekea upotevu wa maji.

Ushauri aliutoa katika mji mdogo wa Ifunda alipotembelea ujenzi wa mradi wa maji wa Ifunda leo.

Mhe Hapi alisema kuwa umefika wakati wa kuanzisha utaratibu wa luku za maji ili mteja alipie huduma ya maji kadri anavyotumia.  Utaratibu huo utaondoa tatizo la watu kukwepa kulipia ankara za maji kwa sababu fedha itakuwa inaingia moja kwa moja kwenye mfumo wa malipo. “Ufike wakati mteja anunue maji kabla hajatumia, huo ndiyo uwe muelekeo kwenye mkoa wetu. Hii itasaidia nidhamu katika matumizi ya maji” alisema Mhe Hapi.

Vilevile, aliitaka Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kutoa mafunzo kwa uongozi wa jumuiya ya watumia maji ili waweze kusimamia vizuri mradi huo na kuepuka migogoro katika usimamizi na uendeshaji wake. “Jumuiya hii ipewe mafunzo ya uendesaji wa mradi huu wa maji, usimamizi wa fedha na utunzaji wa kumbukumbu” alisisitiza Mhe Hapi.

Katika taarifa ya ujenzi wa mradi wa maji Ifunda, iliyosomwa na mhandisi wa maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Andrew Kisalo alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuboresha huduma ya maji safi baada ya mradi uliokuwepo kuwa na mapungufu katika uzalishaji wa maji na kushindwa kuhudumia wakazi wapatao 5,649 wa kijiji cha Ifunda na Bandabichi. Alisema kuwa mradi huo unagharamiwa na WARIDI kwa shilingi 214,161,642 na mchango wa wananchi shilingi 9,550,000.

Akiongelea changamoto za mradi huo, alizitaja kuwa ni kiwango kidogo cha umeme kutoka katika transfoma iliyopo kuzalisha umeme kwa kuhudumia mradi na jamii kiasi kinachopelekea pampu kushindwa kupampu maji wakati wa mchana na kulazimika kupampu wakati wa usiku kwa nyakati tofauti. Nyingine aliitaja kuwa wateja binafsi waliounganishiwa maji kukaidi zoezi la kuakikiwa upya na kuchukua fomu za kusajili ili kuingia katika utaratibu wa kulipia. Baadhi ya viongozi wa jumuiya ya watumiaji maji kutokumudu kutimiza wajibu wao katika kuusimamia mradi wa maji.

Mradi wa maji wa Ifunda ulibuniwa ili kutekeleza mpango wa kuboresha huduma ya maji kwa wakazi wa kijiji cha Ifunda na Bandabichi ukiwa ni miongoni mwa miradi ya matokeo ya haraka inayofadhiriwa na wadau wa kimarekani chini ya shirika la WARIDI, ukijengwa na mkandarasi GEK-Girison Investment Co Ltd.  

=30=

Matangazo

  • BURIANI HAYATI RAIS JOHN POMBE MAGUFULI March 19, 2021
  • Ratiba ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa Mwezi Machi March 08, 2019
  • Ratiba ya Mh. Mkuu wa Mkoa kwa Mwezi Aprili April 04, 2019
  • Rc Hapi Aanza Ziara Kukagua Miradi Halmashauri Za Iringa August 27, 2019
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKUU WA MKOA QUEEN SENDIGA AWATAKA WAKUFUNZI WA MRADI WA SEQUIP KUFWATA KILICHO WALETA .

    June 22, 2022
  • RC SENDIGA AONGOZA KIKAO KAZI CHA KUFANYA TATHIMINI UTENDAJI WA TASAF.

    June 21, 2022
  • CCM MKOA WA IRINGA WANAFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO MKUBWA NA SERIKALI YA MKOA NDIO MAANA KUNAUTULIVU MKUBWA NA KASI KUBWA YA MAENDELEO.

    June 17, 2022
  • SENEDA AWAPONGEZA MAAFISA ELIMU WOTE NDANI YA MKOA WA IRINGA KWA ONGEZEKO LA UFAULU MZURI KITAIFA.

    June 14, 2022
  • Tazama zote

Video

MAFANIKIO YA TARURA NA TANROADS MKOA WA IRINGA YAPAMBA MBOTO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.