• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC HAPI APOKEA NA KUKABIDHI KOMPYUTA 20

Posted on: October 17th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, IRINGA

Manispaa ya Iringa imetakiwa kujenga na kuimarisha vipawa vya wanafunzi kupitia somo la kompyuta ili waweze kuendana na uchumi wa viwanda.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi alipokuwa akipokea na kukabidhi kompyuta 20 ambazo ni ufadhili wa mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa, Mhe Rita Kabati leo katika ukumbi wa shule ya sekondari Lugalo.

Mhe Hapi alisema kuwa dunia ya leo inahitaji watu wenye vipawa vingi, miongoni mwa vipawa hivyo ni elimu ya kompyuta. Kompyuta ni moja ya htaji la msingi kumuwezesha binadamu kuishi. “Nipo hapa kwa ajili ya kupokea na kukabidhi kompyuta 20, kati ya hizo, kompyuta 11 ni kwa ajili ya shule za Halmashauri ya Manispaa na zinazobaki kwa ajili ya shule za Halmashauri nyingine katika mkoa wa Iringa. Kompyuta hizi zitoe nafasi kwa wanafunzi wetu kujifunza somo la kompyuta. Dunia ya leo inahitaji watu wenye vipawa vingi ikiwa ni pamoja na kompyuta”. Aidha, alimuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa kuhakikisha kompyuta hizo zinatunzwa na zinatumika vizuri kwa kazi iliyokusudiwa. Kama wataalam wa kufundisha kompyuta ni wachache, wafundishe kwa utaratibu wa mzunguko ili elimu hiyo iwafikie wanafunzi wengi zaidi, alishauri Mhe Hapi.

Wakati huohuo, Mbunge wa viti maalum, Mkoa wa Iringa, Mhe Rita Kabati amepongeza utayari wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika shughuli za maendeleo na kumuita kuwa ni mzalendo na mtu wa kazi. Aidha, aliongelea tatizo la mawasiliano kupitia minara ya simu katika Mkoa wa Iringa kuwa linawaathiri wanawake zaidi. “Mimi sipendi wanawake wapande kwenye minara kutafuta mtandao. Mkoa wa Iringa bado unahitaji minara ya mawasiliano ya simu. Nitandelea kuwasiliana na mamlaka husika kuhakikisha minara zaidi inajengwa Mkoani Iringa” alisema Mhe Kabati.

Katika hafla ya kupokea na kukabidhi kompyuta 20, Mkuu wa Mkoa alizindua shindando la sayansi kwa shule za Mkoa wa Iringa.

=30=  



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.