• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC HAPI AAGIZA MUFINDI KUSIMAMIA UKUSANYAJI MAPATO

Posted on: August 14th, 2018


Na. Ofisi ya Mkuu wa mkoa

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, mhe Ally Hapi ameiagiza Wilaya ya Mufindi kusimamia ukusanyaji wa mapato ya serikali na kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Agizo hilo alilitoa alipokuwa akiongea na wafanyakazi wa Wilaya ya Mufindi katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Mufindi katika siku ya pili ya ziara yake ya wilaya kwa wilaya mkoani Iringa.

Mhe Hapi aliitaka Wilaya ya Mufindi kuendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato ya serikali. “Asilimia 78 ya ukusanyaji wa mapato bado ni ndogo. Nataka halmashauri zote za Iringa zisishuke asilimia 90 ya ukusanyaji wa mapato ya serikali. Mamlaka ya mapato Wilaya ya Mufindi ongezeni kasi ya kukusanya mapato ya serikali” alisema mhe Hapi. Katika kusogeza huduma ya ukusanyaji mapato karibu na wananchi, aliwataka wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa kusogeza vituo vya kukusanyia mapato maeneo ya kimkakati karibu na wananchi. Aliwataka kuweka nguvu kwenye kubuni vyanzo vipya vya mapato ili fedha inayokusanywa ipelekwe kwenye huduma za wananchi.

Mkuu wa Mkoa aliziagiza halmashauri za mji Mafinga na Wilaya ya Mufindi kutenga fedha za mikopo ya vijana na akina mama asilimia 10. Alisema kuwa serikali ilishatoa maelekezo kuwa fedha hizo zikopeshwe bila riba na zitolewe zote asilimia 10 ya mapato ya halmashauri. “Katika kukopesha vijana, msikopeshe fedha ghafi, kopesheni mashine za viwanda vidogovidogo” alisema mhe Hapi. Vilevile, aliwataka kuepuka kukopesha vikundi vilevile badala yake kukopesha vikundi vipya.

Akiongelea ujenzi wa viwanda, mkuu wa Mkoa aliitaka Wilaya ya Mufindi kutenga maeneo ya uwekezaji wa viwanda. Alielekeza maeneo hayo yatengwe pamoja na maeneo ya makazi ya wafanyakazi wa viwanda hivyo. “Ili maeneo ya uanzishaji viwanda hivyo yawe na mvuto, mjipange kufikisha huduma za msingi kama maji, umeme, barabara. Watu wa EPZ watafutwe waje walione eneo hilo na kuona namna ya kuliendeleza” alisema mhe Hapi.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa yupo katika ziara ya wilaya kwa wilaya kujitambulisha na kutoa muelekeo wa Iringa mpya anayoitaka katika uongozi wake kwa wafanyakazi.

=30=

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.