• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RAS WAMOJA AWATAKA WANAFUNZI WANUFAIKA WA TASAF KUSOMA KWA JUHUDI

Posted on: December 6th, 2017

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Wanafunzi wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini (TASAF) wametakiwa kusoma kwa juhudi na maarifa na kuacha utukutu ili wawe raia wenye mchango kwa Taifa lao.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipofanya ziara ya kutembelea wanufaika wa TASAF kupitia elimu katika Manispaa ya Iringa.

Ayubu alisema “serikali tunategemea msome kwa bidii sana na msiwe watukutu. Nia ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dr. John Magufuli ni kujenga msingi imara kwa wananchi wake kupitia elimu. Tunataka kuwa na Taifa lenye wananchi wenye uwezo wa kufanya kazi na kujitegemea”. Alisema kuwa wanafunzi hao wamepata fursa ya kupata elimu bila malipo na fedha kupitia TASAF kwa ajili ya kununua mahitaji muhimu ya shule.

Katibu Tawala Mkoa, alisema kuwa wapo wazazi wanaozembea kuwanunulia watoto wao wanufaika wa TASAF wafuatiliwe ili waweze kutimiza wajibu huo. Alisema kuwa lengo la fedha hizo ni kuwawezesha watoto hao kupata sare za shule, madaftari, kalamu na mahitaji mengine muhimu ya shule. “Hapa lazima ifahamike kuwa, fedha hizi si za wazazi wla walezi, ni fedha kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wanufaika kupata mahitaji yao ya lazima kwa ajili ya shule ili wasijisikie wanyonge pindi wanapokuwa shuleni” alisisitiza Ayubu.

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa alifanya ziara maalum ya ufuatiliaji kwa wanafunzi wanufaika wa mpango wa TASAF kupitia elimu katika Manispaa ya Iringa kujifunza changamoto zinazowakabili. Katika ziara hiyo aliambatana na mratibu wa TASAF Mkoa, afisa mipango, mhasibu, mkaguzi wa ndani na afisa habari.

=30=






Matangazo

  • BURIANI HAYATI RAIS JOHN POMBE MAGUFULI March 19, 2021
  • Ratiba ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa Mwezi Machi March 08, 2019
  • Ratiba ya Mh. Mkuu wa Mkoa kwa Mwezi Aprili April 04, 2019
  • Rc Hapi Aanza Ziara Kukagua Miradi Halmashauri Za Iringa August 27, 2019
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKUU WA MKOA QUEEN SENDIGA AWATAKA WAKUFUNZI WA MRADI WA SEQUIP KUFWATA KILICHO WALETA .

    June 22, 2022
  • RC SENDIGA AONGOZA KIKAO KAZI CHA KUFANYA TATHIMINI UTENDAJI WA TASAF.

    June 21, 2022
  • CCM MKOA WA IRINGA WANAFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO MKUBWA NA SERIKALI YA MKOA NDIO MAANA KUNAUTULIVU MKUBWA NA KASI KUBWA YA MAENDELEO.

    June 17, 2022
  • SENEDA AWAPONGEZA MAAFISA ELIMU WOTE NDANI YA MKOA WA IRINGA KWA ONGEZEKO LA UFAULU MZURI KITAIFA.

    June 14, 2022
  • Tazama zote

Video

MAFANIKIO YA TARURA NA TANROADS MKOA WA IRINGA YAPAMBA MBOTO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.