• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MUITIKIO WANAUME KUPIMA VVU SI WA KURIDHISHA

Posted on: July 9th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Watanzania zaidi ya asilimia 50 ya watu wanaoishi na VVU hawajui kuwa wanaishi na VVU mchango mkubwa ukitokana na kiwango cha wanaume kutojitokeza kupima VVU.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua kikao cha maandalizi ya kampeni ya Furaha Yangu, ya kupima VVU na kuanza dawa mapema, kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Masenza alisema “kitaifa inakadiriwa kuwa asilimia 52.2 ya watu wanaoishi na VVU hawajui kuwa wanaishi na VVU. Kwa kiasi kikubwa hali hii inachangiwa na wanaume ambao kiwango chao cha upimaji kiko chini sana, ambacho ni asilimia 45.3 ukilinganisha na kinamama ambao kiwango chao ni asilimia 55.9 kulingana na matokeo ya utafiti wa viashiria vya VVU/UKIMWI (Tanzania HIV Impact Survey 2016/17)”. Umefika wakati kampeni za mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU zielekezwe katika kuwahamasisha wanaume/vijana wa kiume kupima VVU na magonjwa mengine, aliongeza. “Najua jambo hili si jepesi kutokana na hulka za akina baba na mazoea ambayo tayari yameshajengeka katika familia nyingi za kiafrika Tanzania ikiwemo” aliongeza Masenza.

Aidha, alitoa wito kwa akina mama walio katika ngazi za uongozi kuhamasika na kuwahamasisha akina mama wanaowaongoza kuwa na agenda moja ya kuwaunga mkono wanaume na vijana wa kiume kuwa tayari kujitokeza kupima afya zao.  

Vilevile, aliwaagiza viongozi ngazi zote mkoani Iringa kutumia kauli mbiu aliyoiongoza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayowalenga wanaume isemayo “Mwanaume Jali Afya Yako, Pima VVU”  ili kuweka msisitizo katika ushiriki wa wanaume katika kampeni hiyo.  

Uzinduzi wa kitaifa wa kampeni ya “Furaha Yangu” umedhihirisha azma ya Serikali yetu ya awamu ya tano ya kuhakikisha kuwa inaimarisha na kuongeza kasi ya mapambano, ili baada ya kuzifikia hizo “tisini tatu” mwelekeo sasa unabaki ni ule wa kufikia zile “sifuri tatu”; kutokuwepo kwa maambukizi mapya ya VVU, kutokuwepo kwa unyanyapaa kwa watu wanaoishi na VVU, na kutokuwepo na vifo vinavyotokana na UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

=30=

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.