• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MUFINDI DC YATEKELEZA MAAGIZO YA SERIKALI KUU

Posted on: May 23rd, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi inatekeleza agizo la serikali ya kuanzisha viwanda nchini ili kujenga Tanzania ya viwanda ifikapo mwaka 2025.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Mufinsi, Allan Benard alipokuwa akisoma risala ya utii ya wananchi wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi kwa Rais Dkt John Magufuli katika uwanja wa mkesha wa Mwenge wa uhuru katika Kata ya Igowole wilayani Mufindi.

Benard alisema kuwa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi inatekeleza maagizo ya serikali katika sekta mbalimbali. “Kabla ya kampeni ya Kiwanda changu Wilaya yangu, halmashauri ilikuwa na jumla ya viwanda 29, vikubwa saba, vya kati vitatu na vidogo 19. Baada ya kampeni hii, viwanda vidogo 11 vimeongezeka na kufanya jumla ya viwanda kuwa 40, ambavyo vinatoa ajira kwa watu 3,788.

Akiongelea utoaji wa chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana, alisema kuwa halmashauri inaendelea na utekelezaji wa chanjo hiyo. Alisema kuwa kamati ya afya ya wilaya na watoa huduma za afya 63 na walimu 192 walipatiwa mafunzo. “Zoezi la utoaji chanjo linaendelea ambapo mpaka sasa jumla ya wasichana 402 (98) kati ya walengwa 442 kwa mwezi wamechanjwa ambapo walengwa 5,308 wanatarajiwa kufikiwa kwa mwaka” alisema Benard.

Mwenge wa uhuru katika halmashauri ya Wilaya ya Mufindi umepitia miradi sita yenye thamani ya shilingi 9,199,229,136. Miradi hiyo ni kuweka jiwe la msingi ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa sekondari ya Igombavanu, kukagua msitu wa kupandwa wa halmashauri na kuzindua ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha mtili. Miradi mingine ni kuzindua ujenzi wa barabara ya lami Kitiru-Itulituli Km 14.977, mradi wa kilimo na mifugo wa wananchi na klabu ya wapinga rushwa sekondari ya Igombavanu.  

=30=



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.