• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mheshimiwa Ally Hapi akemea vikali kwa baadhi ya Taasisi za Serikali zinazogeuka kuwa mwiba kwa Wawekezaji.

Posted on: December 19th, 2019

Mheshimiwa Hapi ameyasema hayo katika kikao cha Wafanyabiasha/Wawekezaji Wilayani Mufindi tarehe 19/1282019 ikiwa ni moja ya majukumu yake katika kuhakikisha Mkoa wa Iringa unakuwa kiuchumi.

Akifungua kikao hicho Mheshimiwa Hapi amesema, kupitia uwekezaji nchi yetu inaweza kuongeza uchumi katika pato la Taifa, hivyo ni muhimu ikafahamika changamoto za wawekezaji, japo zingine zinafahamika. Dhamira ya Mkoa wa Iringa ni kutatua matatizo na vikwazo mbalimbali vinavyowakabili wawekezaji ili kumsaidia Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli katika kufanikisha kuleta wawekezaji nchini.

Mheshimiwa Hapi katika kukemea amesema, kuna baadhi ya Taasisi za Serikali zimekuwa mwiba kwa wawekezaji kwa kufanya kazi bila kufuata taratibu na kanuni za nchi. Baadhi ya Taasisi hizo huenda kwenye viwanda na kukusanya kodi wakiwa wameshika bunduki, Mheshimiwa Rais amepiga marufuku nchi nzima, kwani wafanyabiashara wamekuwa wakitishika sana, wanapoona bunduki hupoteza ufanisi wa kazi.

Wawekezaji hawa wakiwa wanahudumiwa vizuri hasa raia wa kigeni, wanaweza kutuma ujumbe kwenye nchi zao kuwa Tanzania ni mahali salama kwa uwekezaji. Ni majukumu ya Mkuu wa Mkoa kusimamia wajibu na sheria za nchi.

Mheshimiwa Hapi ameelekeza kuwa, kama Taasisi inakwenda kukagua viwanda, ni lazima Mkuu wa Wilaya husika apate taarifa, na watoe sababu wanakwenda kufanya nini, pia mwenye kiwanda lazima ajulishwe. Ikigundulika kuna makosa madogo huwa wanasema ‘funga kiwanda baada ya masaa 24’, sasa ni marufuku kiwanda kufungwa hadi Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa atakapojiridhisha kufunga kiwanda hicho kwa sababu husika.

Pia Mheshimiwa Hapi ameutaka uongozi wa TFS kutoa vibali vya kudumu kwa wawekezaji wenye sifa na vigezo na siyo kwa watu wachache tu kama ilivyo sasa hivi.

Amesisitiza kuwa, Halmashauri zote zitenge maeneo kwa ajili ya viwanda kwa wawekezaji, kuanzia sasa kila Mkurugenzi wa Halmashauri katika vikao vyetu ataeleza ametenga vipi maeneo hayo.

Akihitimsha kikao hicho Mheshimiwa Hapi amesema, Wilaya ya Mufindi ina neema kubwa ya uwekezaji viwanda, wasaidie wageni ili wawekeze kwa wingi bila bughudha. Pia amewaonya watu wa mazingira kufanya opereshini ya kukagua mifuko ya plastiki ambayo kwa sasa inatumika kwa kasi sana kama vifungashio.


Imetolewa na Ofisi ya Habari Mkoa,

Humphrey Kisika.


Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.