• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Queen Sendiga Azindua Kampeni Ndogo ya Chanjo ya UVIKO-19

Posted on: July 20th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Iring Mhe. Queen Cuthbert Sendiga amezindua kampeni ndogo ya chanjo ya UVIKO-19 Mkoani Iringa ambayo ina lengo la kuongeza kasi ya uchanjaji.

Mhe.Sendiga amesema kuwa Mkoa wa Iringa ni moja kati ya mikoa inayotekeleza zoezi la uchanjaji chanjo ya UVIKO-19 ili kuwakinga wananchi dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19. Chanjo za UVIKO-19 zimeidhinishwa na shirika la Afya Duniani (WHO) kwa ajili ya Mapambano ya Ugonjwa wa UVIKO-19. Chanjo hizi zinapunguza uwezekano wa mtu kuambukizwa ugonjwa UVIKO-19 na hata mtu akiambukizwa hupunguza uwezekano wa kulazwa na kufa.

Aidha Mkuu wa mkoa wa Iringa amesema Mpaka sasa mkoa wa Iringa Umepokea chanjo za aina tano ambazo ni Janssen, Pfizer, Moderna, Sinovac na Sinopharm. Chanjo hizi zimeidhinishwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kutumika nchini.

Aidha ameendelea kwa kusema kuwa, Baada ya Mafanikio makubwa kupatikana katika awamu ya kwanza ya mpango jumuishi harakishi wa uchanjaji chanjo ya UVIKO-19 Serikali kupitia Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI ilizindua Awamu ya pili ya mpango shirikishi na harakishi wa uchanjaji chanjo ya UVIKO-19 mnamo tarehe 22 Desemba 2021 Mkoani Arusha. Lengo la mpango huu ni kuongeza kasi ya uchanjaji kuelekea kufikia asilimia 70 ya watanzania ifikapo Desemba 2022.

“Kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari 2022 hadi tarehe 18 Julai 2022 mkoa umepokea chanjo za UVIKO-19 495,307 (Janssen 238035, Pfizer 161650, Sinopharm 51832, Sinovac 31500 na Moderna 12290).  Uchanjaji chanjo ya UVIKO-19, umendelea kufanyika na kwa sasa mkoa unatekeleza kampeni ya uchanjaji chanjo ya UVIKO-19 iliyoanza tarehe 1 Juni 2022 hadi 30 Septemba 2022. Hadi kufikia tarehe 18 Julai 2022 mkoa umechanja jumla ya watu 133,497 sawa na asilimia 19.8 ya walengwa 671,974.” Mhe. Queen Sendiga.

Na hivyo Kuanzia tarehe 20 Julai 2022 hadi kufikia 24 Julai 2022 tutakuwa na kampeni ndogo ya uchanjaji chanjo ya UVIKO-19 inayolenga kuchanja wateja 100,000. Kufikia malengo haya kila halmashauri inatakiwa kuchanja wateja zaidi ya 2500 kwa siku.

Mhe. Queen Sendiga amemaliza kwa kuwahamasisha wananchi wote walio na umri wa miaka 18 na kuendelea ambao bado hawajapata chanjo ya UVIKO-19 wapate chanjo hii katika kipindi hiki cha kampeni. Pia wananchi waliopata dozi ya kwanza wafike katika vituo vya kutolea huduma za chanjo kupata dozi ya pili ili miili yao iweze kuwa na kinga kamili.

Kwa chanjo ya Sinopharm dozi ya pili inatolewa siku 28 baada ya kupata dozi ya kwanza na kwa chanjo ya Pfizer au Moderna dozi ya pili inatolewa kuanzia siku ya 21 hadi 28 baada ya kupata dozi ya kwanza. Kwa sasa mkoa una jumla ya vituo 259 vinavyotoa huduma za chanjo. Pamoja na uchanjaji katika vituo watoa huduma wanatumia huduma za mkoba ili kuwafikia wananchi popote walipo.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.