• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MKOA WA IRINGA UMEONGEZA KIWANGO CHA UFAULU KWA 0.27%.

Posted on: December 26th, 2017

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa umefanikiwa kuongeza kiwango cha ufaulu kwa watahiniwa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2017 kwa asilimia 0.27 na kushika nafasi ya nne kitaifa.


Kauli hiyo ilitolewa na mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi wa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2018 mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu katika hotuba yake ya ufunguzi kwenye ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.


Ayubu alisema “watahiniwa 20,606 (wavulana 9,513 na wasichana 11,093) sawa na asilimia 83.14 wamefaulu mtihani huo. Hali kadhalika walioshindwa kufaulu mtihani huo ni 4,178 ikiwa wavulana 1,908 na wasichana 2,270 sawa na asilimia 16.86.

Kiwango hiki cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 0.27 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka jana ambapo ufaulu ulikuwa ni 82.87% ninapenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza wadau wote wa elimu katika Mkoa wetu ambao mchango wao ni mkubwa kwa ongezeko hili la ufaulu na kuufanya Mkoa wetu kuwa wa Nne kitaifa kati ya mikoa 26 ya Tanzania bara”.


Ayubu ambaye pia ni Katibu Tawala Mkoa wa Iringa alisema kuwa ongezeko hilo la ufaulu ni jambo jema na kutahadharisha kuwa linaibua changamoto ya uhitaji mkubwa wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari. “Ongezeko la ufaulu ni jambo jema kwetu lakini linaibua changamoto ya uhitaji mkubwa wa vyumba vya madarasa katika shule zetu za sekondari au ujenzi wa shule mpya za Sekondari ili kuweza kuwachukua wanafunzi wote waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza” alisema Ayubu.


Aidha, aliwataka wajumbe kuangalia jinsi ya kuongeza vyumba vya madarasa au kujenga shule za sekondari maeneo ambayo yamekuwa na wanafunzi wengi wanaofaulu hasa mijini. Aliongeza kuwa ongezeko la ujenzi wa vyumba vya madarasa liambatane na uongezaji wa meza na viti ili kuhakikisha wanafunzi wote wanapata meza na viti.


Mkoa wa Iringa ulikuwa na watahiniwa 24,905 waliosajiliwa kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2017, kati yao wavulana 11,490 na wasichana 13,415 katika shule 481.

=30=




Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.