• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Michezo Mahala pa Kazi iimarishe Afya za Wafanyakazi

Posted on: April 24th, 2018


Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,

Michezo mahala pa kazi itumike kujenga na kuimarisha afya za wafanyakazi ili waendelee kutoa huduma nzuri kwa wananchi nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika hotuba yake ya uzinduzi wa michezo ya Mei Mosi kitaifa mwaka 2018 iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Samora mjini Iringa na kusomwa na afisa elimu mkoa wa Iringa, Mwl Majuto Njanga.

Masenza alisema kuwa michezo mahala pa kazi ni muhimu sana katika kusaidia kujenga na kuimarisha afya za wafanyakazi. Alisema kuwa afya za wafanyakazi zinapoimarika zinawawezesha kutoa huduma bora kwa wananchi pamoja na kuongeza tija mahala pa kazi. “Mfanyakazi legelege hatoweza kuzalisha tija au kutoa huduma bora iliyotukuka kwa sababu ya mwili wake kudumaa kwa kukosa mazoezi” alisema Masenza. Aliongeza kuwa michezo mahala pa kazi husaidia kujenga mahusiano mema miongozi mwa wafanyakazi.

Mkuu wa mkoa alisikitishwa na kupungua kwa timu shiriki katika mashindano ya Mei Mosi, 2018 ambapo timu zimepungua kutoka 15 hadi kufikia timu 10. “Nawalaumu sana viongozi wote ambao wameingia woga na kuwanyima fursa wanamichezo wafanyakazi kuja kushiriki kwenye michezo hii ya Mei Mosi kitaifa ambayo mhe Rais ndiye mgeni rasmi katika maonesho haya”.

Aidha, alitoa rai kwa viongozi kuhakikisha michezo inafanyika mahala pa kazi na timu hizo zishiriki katika michezo ya Mei Mosi kitaifa ikiwepo michezo ya SHIMIWI, SHIMMUTA, SHIMISEMITA na BAMMATA. Aliitaka TUCTA kufikisha taarifa kwa menejimenti za timu mbalimbali ili zishiriki kwenye michezo ya Mei Mosi kitaifa.

Akiongelea kaulimbiu ya michezo ya Mei Mosi mwaka 2018 inayosema “Tanzania ya viwanda swadaktaa…kwa ukuzaji wa ajira sambamba na uhamasishaji wa michezo kazini”, kaimu makamu mwenyekiti wa kamati ya michezo ya Mei Mosi taifa, Joyce Benjamin alisema kuwa wanaimani kubwa kuwezekana kwa Tanzania ya viwanda nchini. Alisema kuwa Tanzania ya viwanda itakwenda sambamba na ukuzaji wa ajira na uhamasishaji wa michezo mahala pa kazi.

Akiongelea kupungua kwa timu za michezo kutoka 15 mwaka 2017 hadi kufikia 10 mwaka huu, Benjamin alisema kuwa wadau wote wakae chini na kutafakari swala hilo kama ni woga au ukosefu wa fedha. “Niseme wazi mhe. Mkuu wa mkoa kwamba mhe. Rais, hajakataza michezo. Hatujasikia akikataza michezo hata siku moja…inawezekana wanamuogopa tu yeye kutumia fedha…lakini kwa nini wamuogope…anachotaka mhe Rais ni uhalisia tu wa matumizi kwenye eneo fulani na si vinginevyo” alisema Benjamin.

Michezo ya Mei Mosi mwaka 2018 imeshirikisha timu kutoka Ikulu, Wizara ya Uchukuzi, MUHAS, Hifadhi ya Ngorongoro, Geita Gold Mine, TRA, TANESCO, TTPL-Morogoro, Ukaguzi na RAS Iringa.

=30=  

 

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.