• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Mh. Hapi amepaokea vifaa kinga kwa ajili ya maambukizi ya covd-19

Posted on: April 30th, 2020

Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Ally Hapi Amepokea Vifaa Kinga vya Kujikinga na Maambukizi ya Ugonjwa wa Covd-19 Kutoka kwa Wadau Mbalimbali tarehe 29/04/2020

Akitoa hotuba fupi ya tukio hilo Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amesema, tuko katika mapambano dhidi ya maambukizi ya covid-19, tuna mambo ya kuzingatia juu ya kujikinga na maambukizi. Kwa mujibu wa Mheshimiwa Waziri Mkuu watu zaidi ya 400 wameambukizwa, pia matumaini yapo kwa wagonjwa zaidi ya 100 wamepona ugonjwa huu na kuruhusiwa kutoka hospitali.

Pia anawaasa wananchi wanaotoa masomo ya ziada kimyakimya kuwa wakibainika watachukuliwa hatua wazazi na watoa masomo hao.

Mkuu wa Mkoa amesema pia katika mazishi watu hawazingatii kukaa umbali wa mita moja kutoka mtu mmoja hadi mwingine, hii itasababisha kuongeza maambukizi haya.

Mkuu wa Mkoa ametoa maagizo kwa Katibu Tawala kuwa, aongee na viongozi wa dini ili kuzingatia tahadhari hii, kwani ugonjwa huu upo na ni hatari sana.

Jeshi la Polisi na Mamlaka za Mitaa nawaagiza kufuatilia wananchi ambao hawachukui tahadhari. Mwananchi yeyote anayekuja kupata huduma katika Ofisi za Umma lazima avae barakoa. Pia amesisitiza kuwa, huu siyo wakati wa kutembeleana bila sababu, nitoe rai kwa wananchi tusisafiri bila sabab za msingi.


Ameongeza kusema kuwa, kuna baadhi ya wafanyabiashara kutokana na maambukizi haya, wamepata fursa ya kuongeza bei kwa bidhaa na chakula kama sukari. Na sasa tupo katika kipindi hiki cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani siyo vizuri kufanya hivyo, kwani Serikali imetoa bei elekezi hivyo kama umeongeza bei yako lazima utakamatwa.

Nachukua nafasi hii kuwashukuru wadau wetu ambao wametusaidia kutupatia vifaa mbalimbali vya kujikinga na maambukizi haya hasa kwa hawa watoa huduma. Vifaa hivyo ni kama magauni, vitakasa mikono, sabuni, matanki kwa ajili ya maji, barakoa na vipima joto. Wadau hao ni ASAS, Sai Villa, Qwihaya, Clinton Foundation na wengine wengi waliojitoa kwa ajili ya kupambana na gonjwa hili hatari kwa jamii, nasema tena ahsanteni sana kwa kutuunga mkono.

Mkuu wa Mkoa alimaliza kwa kusema, natoa rai kwa wananchi wanaotoa taarifa za upotoshaji kuhusu ugonjwa wa Corona, nafurahi kuona Jeshi la Polisi lipovizuri katika kuwafuatilia watu hawa na kuwachukulia hatua, nawapongeza sana, endeleeni kufanya kazi vizuri kwa weledi.

Pia Mheshimiwa Hapi ameendelea kuwasisitiza wananchi kuchukua tahadhari juu ya Covid-19.

Imetolewa na:

Ofisi ya Habari Mkoa.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.