• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MASENZA AWATAKA WAFANYA BIASHARA KULIPA KODI

Posted on: February 21st, 2018

Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Serikali mkoani Iringa imewataka wafanyabiashara wote kulipa kodi kwa mujibu wa sheria ili serikali iweze kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akisalimia wachimbaji wadogo wa mgodi wa nyakavangala katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Nyakavangala kilichopo wilayani Iringa alipokuwa akiongea na wachimbaji wadogo wakati wa ziara ya naibu waziri wa Madini, Dotto Biteko mkoani Iringa jana.

Masenza alisema “katika Mkoa wangu, siruhusu mtu yeyote kufanya biashara bila kulipa kodi. Lazima kulipa kodi. Kodi ndiyo inajenga zahanati, kodi ndiyo inajenga shule na miundombinu yote na kodi ndiyo inalipa mishahara”. Alisema kuwa utamaduni wa kulipa kodi ndiyo utawezesha ujenzi wa barabara ya kuelekea katika machimbo ya Nyakavangala kwa kiwango kinachoridhisha.

Aidha, pamoja na kuwapa pole wachimbaji wa dhahabu wa Nyakavangala kufuatia vifo vilivyotokana na ajali zilizotokea siku za nyuma katika mgodi huo, aliwataka kuzingatia kanuni za usalama. “Sitaki vifo katika Mkoa wangu. Lazima kanuni za usalama zizingatiwe wakati wa uchimbaji wa dhahabu”. Alisema kuwa ushauri wa wakaguzi wa madini uzingatiwe ili machimbo ya Nyakavangala yawe eneo salama kwa wachimbaji wadogo mkoani Iringa.

Wakati huohuo, mkuu wa Mkoa wa Iringa alimuagiza mkuu wa Wilaya hiyo kwenda kuwasikiliza wananchi waliojaribu kubeba mabango katika ziara ya naibu waziri wa Madini ili kufahamu hoja zao na kuzitafutia ufumbuzi.

Akiongea katika majumuisho ya ziara yake yaliyofanyika katika ofisi ya mkuu wa Mkoa, naibu waziri wa Madini, Dotto Biteko alisema kuwa nchi imempata kiongozi anayethubutu kuhakikisha madini yanawanufaisha watanzania. “Rais, Dr John Magufuli ana dhamira ya dhati kuyafanya madini yawanufaishe wananchi wa Tanzania na kuchangia katika pato la taifa. Dhamira yake ni kuona madini yanawanufaisha wachimbaji wadogo na hatimae kufikia hatua ya uchimbaji mkubwa” alisema Biteko.

=30=



Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.