• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru arizishwa na ubora wa Miradi ya Halmashauri ya Mufindi

Posted on: May 24th, 2018

Na. Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji -Mufindi

Jumla ya Miradi 06 yenye thamani ya shilingi bilioni 9.199 imezinduliwa, kuwekewa mawe ya msingi pamoja na kukaguliwa na Mwenge wa Uhuru, ulipokimbizwa katika Halmshauri ya Wilaya ya Mufindi, huku wakimbiza Mwenge kitaifa wakiridhishwa  na viwango vya miradi husika na kutanabaisha kuwa vinaendana na thamani ya fedha zilizotumika.

 Ukiwa katika Halmashauri  ya Wilaya ya Mufindi  Mwenge wa Uhuru  umeweka jiwe la msingi katika ujenzi wa vyumba vya Madarasa   Sekondari  ya Igombavanu, umezindua klabu ya wapinga rushwa katika Shule ya Sekondari Igombavanu,  ujenzi wa zahanati ya Kijiji pamoja na kukagua mradi wa hifadhi ya mazingira katika msitu wa kupandwa wa Halmashauri  Kijiji cha Mtili,  umezindua ujenzi wa Barabara ya lami Kitiru- Itulituli yenye urefu wa Kilomita 14.972, na mradi wa kilimo na mifugo wa mwananchi  kata ya Igowole.

Akizungumza wakati wa kutoa ujumbe wa Mwenge,kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu. Charles Francis Kabeho, amewahamasisha wananchi kuwekeza katika elimu kwa  kugharamia mahitaji muhimu ya Watoto wao, kama mavazi, viatu, Madaftari  sanjari na kuchangia mchango wa Chakula cha mchana kwa wanafunzi wa kutwa  chini ya ujumbe mkuu wa mbio za Mwenge 2018 “ELimu ni Ufunguo wa Maisha Wekeza Sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu”

Aidha, ameendelea Kuhamasisha kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, VVU/UKIMWI, dawa za kulevya na mapambano dhidi ya Malaria.

“Maambukizi ya UKIMWI yameendelea kuwa tatizo kubwa katika Mkoa wa Iringa, mkiongozwa na Mkoa wa Njombe wenye asilimia 11.4, wakati ninyi mnashika nafasi ya pili kitaifa kwa kuwa na maambukizi ya asilimia 11.3 hivyo, inatupasa tuchukue hatua za kubadili tabia kwani hali hii ikiendelea hivi ni hatari kwa maendeleo ya Taifa’’ alisema Kabeho

Kwa Upande Wake Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Jamhuri William, Kupitia risala ya utii  kwa mkuu wa nchi, amemhakikishia  Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwamba, Wilaya yake, itaendelea kutekeleza  Maagizo mbalimbali ya Serikali ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa viwanda, usimamizi wa Mbolea ya ruzuku, kuokoa mifumo ya kiikolojia ya bonde la Mto Ruaha mkuu pamoja  na suala la Waalimu Kutojihusisha na michango ya Wazazi Shuleni .

Mkesha wa Mwenge wa Uhuru uliambatana na zoezi la upimaji wa maambukizi ya virusi vya UKIMWI na katika upimaji huo,  jumla ya watu 435 walijitokeza kujua Afya zao, kati yao wanaume ni 232 na Wanawake ni 203 ambapo katika zoezi hilo ni watu 04 tu ndio waligundulika kuwa na maabukizi ikiwa ni Wanawake 02 na Wanaume 02.


=30=

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.