• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

IRINGA YAWAASA WAKANDARASI KUJIPANGA SAWASAWA

Posted on: February 26th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Serikali mkoani Iringa imewataka wakandarasi wa ujenzi wa miradi ya barabara kujipanga sawasawa katika kutekeleza miradi ya ujenzi ili idumu kwa muda mrefu.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika hotuba yake ya halfa ya utiaji saini mikataba baina ya TARURA na wakandarasi katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa Mkoa jana.

Masenza aliwataka wakandarasi wote walioshinda zabuni za ujenzi wa barabara katika Mkoa wa Iringa kujipanga sawasawa. “Serikali imewekeza pesa nyingi katika ujenzi wa barabara kwa lengo la kujenga na kuimarisha barabara ili mwananchi aweze kunufaika na barabara hizo. Tumesikia katika taarifa ya mratibu wa TARURA Mkoa wa Iringa kuwa gharama za ujenzi wa barabara ni shilingi bilioni 3.56” alisema Masenza. Aidha, alitumia hafla hiyo kuwataka wakandarasi wote kufanya kazi kwa kuzingatia muda uliopangwa na viwango vya ubora wa kazi. Serikali haitamvumilia mkandarasi yeyote atakayefanya kazi chini ya muda uliopangwa kwenye mkataba wala kazi iliyofanywa chini ya kiwango, aliongeza Masenza.

Katika kuhakikisha ubora wa kazi za ujenzi, mkuu wa mkoa wa Iringa aliwataka mameneja wa TARURA wa halmashauri kuwasimamia wakandarasi ili watekeleze majukumu yao. “Serikali imeajiri mameneja wa TARURA katika halmashauri. Jukumu kubwa la mameneja hawa ni kuwasimamia wakandarasi ili watekeleze wajibu wao. Hivyo, mameneja wa halmashauri pia mjipange sawasawa kuhakikisha ubora na thamani ya fedha inapatikana” alisisitiza mkuu wa mkoa.

Mkuu wa mkoa alitoa wito wa kulipwa kwa wakati pindi wakandarasi watakapotimiza wajibu wao kwa kuzingatia vigezo vya ubora kwa mujibu wa mikataba iliyosainiwa. Alisema kuwa kuna wakati malipo ya wakandarasi yamekuwa yakicheleweshwa kutokana na uzembe na kutofuata taratibu. “Utekelezaji huo utawafanya kuongeza morari ya kazi na pia kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima kwa Serikali” alisema mkuu wa mkoa.

Awali mratibu wa TARURA Mkoa wa Iringa, mhandisi Juma Wambura katika taarifa yake alisema kuwa TARURA Mkoa wa Iringa ilitangaza miradi ya barabara za halmashauri zote za Mkoa jumla ya zabuni 26 zenye thamani ya shilingi bilioni 6.5. “Leo utaishuhudia mikataba 18 ikisainiwa na wazabuni walioshinda baada ya mchakato mzima wa manunuzi kukamilika yenye thamani ya shilingi bilioni 3.56. Mhe. mkuu wa mkoa, mikataba takribani 8 itasainiwa baadae baada ya taratibu za manunuzi kukamilika” alisema mhandisi Wambura.

Mratibu huyo alisema kuwa lengo la TARURA ni kufanikisha dhima kuu ya Serikali kuwa miundombinu ya barabara inaboreshwa na kusonga mbele kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi ili iweze kuboresha uchumi wa wananchi.

TARURA mkoa wa Iringa inahudumia mtandao wa barabara wenye jumla ya Kilomita 4,601.25 inayojumuisha halmashuri tano za Manispaa, halmashauri za wilaya za Iringa, Kilolo, Mufindi na Mji wa Mafinga.

=30=



Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.