• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

IRINGA YAPONGEZWA USIMAMIZI UJENZI WA HOSPITALI WILYA KILOLO

Posted on: January 29th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Iringa imepongezwa kwa usimamizi makini unaozingatia thamani ya fedha katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kilolo unaoendelea.

Pongezi hizo zilitolewa na makamu mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya utawala na serikali za mitaa, Mwanne Mchemba alipokuwa akiongea na wataalam wa Mkoa wa Iringa na Wilaya ya Kilolo katika kumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo baada ya kamati yake kukagua ujenzi wa hospitali hiyo hivi karibuni.

Mchemba alisema kuwa ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Iringa imefanya kazi nzuri kusimamia ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kilolo. “Najua mipango mizuri ya ujenzi wa hospitali hii mliiratibu vizuri tangu mwanzo ndiyo sababu ujenzi unaenda vizuri. Kamati yangu imeridhishwa na hatua ya ujenzi kwa kuzingatia thamani ya fedha” alisema Mchemba. Alipongeza wazo hilo kuwa linalenga kuboresha afya za wananchi wa Wilaya ya Kilolo na taifa kwa ujumla kwa kuwapatia huduma bora za afya.

Mchemba aliishauri ofisi ya Rais TAMISEMI kutoa kipaumbele katika ujenzi wa chumba cha upasuaji na chumba cha kuhifadhia maiti. Alisema kuwa ujenzi wa majengo hayo utasaidia kuiwezesha hospitali hiyo kuanza ikiwa na maeneo muhimu ya utoaji huduma. Aidha, alielekeza hospitali hiyo kupatiwa gari la wagonjwa. “Kutokana na jiografia ya Wilaya ya Kilolo ni muhimu hospitali ya Wilaya kupewa gari la wagonjwa. Gari hilo ni muhumu sana kwa sababu litasaidia kuokoa maisha ya wananchi watakaohitaji huduma ya haraka na dharura hospitali hapo” alisema Mchemba.  

Awali katika taarifa ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kilolo iliyosomwa na mganga mkuu wa Wilaya, Dr. Mohamed Mang’una alisema kuwa mradi huo ulianza kwa gharama ya shilingi 259,451,899 kugharamia ujenzi awamu ya kwanza na ya pili. Alisema kuwa kupitia ruzuku ya maendeleo ya serikali za mitaa kwa mwaka 2011/2012 zilitolewa shilingi 145,744,500 na mwaka 2012/2013 zilitolewa shilingi 113,707,399 kujenga jengo la wagonjwa wa nje.

Hospitali ya Wilaya ya Kilolo imelenga kuhudumia wakazi wanaokadiriwa kuwa 229,146 kutokana na sense ya watu na makazi ya mwaka 2012.

=30=

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.