• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

IRINGA WATAKIWA KUSHIRIKI KAMPENZI YA FURAHA YANGU

Posted on: July 21st, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Wananchi mkoani Iringa wametakiwa kushiriki kikamilifu katika uzinduzi wa kampeni ya furaha nyangu ya kupima virus vya ukimwi na kuanza dawa mapema za kufubaza virus vya ukimwi.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, amina masenza alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu ya kupima virus vya ukimwi na kuanza tiba mapema katika ofisi ya mkuu wa mkoa jana.

Masenza alisema kuwa ni muhimu kwa wananchi wote kujitokeza kushiriki katika uzinduzi wa kampeni hiyo. “Nitoe wito kwa Wananchi wote kushiriki kikamilifu katika uzinduzi na mwitikio wa Kampeni hii muhimu kwa mkoa wetu. Baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo, huduma zitaendelea kutolewa katika hospitali zote, vituo vyote vya afya na Zahanati zote mkoani Iringa” alisema masenza.

Kampeni hii ya Kupima na kuanza kutumia dawa za kufubaza makali ya VVU mapema inakwenda na kaulimbiu ya ujumla isemayo “Furaha Yangu” – Pima, Jitambue, Ishi inaanza kwa kuwalenga Wanaume na kisha makundi mengine ya watu walio katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi ya VVU, aliongeza. Aliyataja makundi hatarishi kuwa ni wasichana walio katika umri wa balehe, wanawake vijana wenye umri wa miaka 15-24, akinamama wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na watoto wao.

Mkuu wa mkoa alisema kuwa uzinduzi wa kampeni ya “Furaha Yangu” unaonesha dhamira ya serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ya kuhakikisha kuwa kasi ya mapambano ya VVU na UKIMWI, inaongezwa ili kufikia zile “tisini tatu” ifikapo mwaka 2020. Alizitaja kuwa ni asilimia 90 ya watu wanaoishi na VVU wawe wamejua hali zao za maambukizo; asilimia 90 ya waliopimwa VVU na kugundulika kuwa wana maambukizo wapatiwe dawa za kufubazamakali ya VVU; na asilimia 90 ya watu wanaotumia dawa wawe wamefubaza VVU.

Kampeni ya “Furaha Yangu” itazinduliwa katika uwanja wa Mwembetogwa mjini Iringa tarehe 24 Julai, 2018 kuanzia saa mbili asubuhi na kuendelea kwa kipindi cha miezi sita ikitarajiwa kuwafikia na kuwapima watu 90,000.

=30=


Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.