• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

IRINGA KINARA TUZO YA RAIS UTUNZAJI MAZINGIRA

Posted on: February 9th, 2018

Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa unatekeleza vizuri mwongozo wa tuzo ya Rais ya utunzaji wa mazingira na uhifadhi ya vyanzo vya maji na Manispaa ya Iringa kushika nafasi ya kwanza kwa Manispaa zote nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akisoma taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Iringa kwa makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan aliye katika ziara ya siku tano mkoani Iringa jana.

Masenza alisema kuwa Mkoa wa Iringa ulipokea na kutekeleza mwongozo wa tuzo ya Rais ya utunzaji wa mazingira na uhifadhi wa vyanzo vya maji. “Katika mwaka 2015 Manispaa ya Iringa ilishika nafasi ya pili, mwaka 2016 ilishika nafasi ya kwanza kwa Manispaa zote Tanzania na mwaka 2017 ilishika nafasi ya tatu kwa Manispaa zote Tanzania” alisema Masenza.

Akiongelea zoezi la upandaji miti na uhifadhi wa mazingira, mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa Mkoa kwa kushirikiana na wadau wa maliasili umeweza kushiriki kikamilifu katika zoezi la upandaji miti na uhifadhi wa mazingira. Aliyataja mafanikio yaliyopatikana kuwa ni

Kuvuka lengo la upandaji miti 55,000,000 kwa msimu 2016/2017 na kupanda miti 56,108,532. Katika zoezi hilo miti 47,766,366 sawa na asilimia 86.84 ilipona. Juhudi nyingine alizitaja kuwa ni kufanya oparesheni maalum ya kubaini na kuondoa wavamizi na mifugo katika hifadhi ya jamii ya Mbomipa wilayani Iringa. Alisema kuwa oparesheni ilifanyika chini ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa ilikamata watuhumiwa 38 wakiwa na mifugo 2,067 na kesi 6 zilifunguliwa mahakamani.

“Halmashauri zote Mkoani Iringa zimetakiwa kuendelea kudhibiti maeneo yote ya hifadhi yasiingizwe mifugo na pia kuendelea kutambua na kupiga chapa mifugo katika maeneo ya Halmashauri ili kuweza kudhibiti mifugo inayoingia bila kufuata taratibu” alisema Masenza.

Kuhusu shindano la usafi wa mazingira lililohusisha halmashauri za majiji, miji na wilaya kwa mwaka 2014, katika ngazi ya Manispaa zote Tanzania, Manispaa ya Iringa ilishika nafasi ya kwanza kitaifa na wilaya ya Mufindi ilishika nafasi ya pili kitaifa wakati kijiji cha Ifunda kikishika nafasi ya kwanza kitaifa.

=30=

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.