• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

HOFU YASABABISHA WENGI KUTOSAJILI VIFO- RC MASENZA

Posted on: June 11th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Hofu ya matukio ya vifo imesababisha watu wengi kutosajili matukio hayo yanapotokea na kupekelea asilimia 17.5 ya usajili nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua kikao cha hamasa kwa viongozi wa Mkoa wa Iringa kuhusu majaribio ya mpango wa usajili wa vifo, kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Masenza alisema kuwa wananchi wamekuwa wakiogopa matukio yanayoambatana na kifo. Woga uliopo ndio unasababisha wananchi wengi kutosajili matukio ya vifo yanapotokea. Woga huyo umesababisha nchi kuwa na wastani wa asilimia 17.5 ya vifo vilivyotokea na kusajiliwa. “Ni imani yangu kwamba tunaenda kubadili hali hii na kama ilivyokuwa kwa usajili wa watoto wadogo ambapo tulikuwa asilimia 11.7 na ndani ya miezi mitatu tukaweza kufika asilimia 100, hivyo naamini tutafanikisha zoezi hili kwa kasi hiyohiyo” alisema Masenza.

Jamii inatakiwa kuhamasishwa kubadili tabia na kuona umuhimu wa kusajili kila tukio la kifo linapotokea. “Wananchi wengi ambao hawana matumizi ya moja kwa moja na cheti cha kifo cha ndugu zao wamekuwa hawafiki RITA kusajili na changamoto kubwa hapa naiona ni kukosa uelewa wa umuhimu wake hivyo kushindwa kubadili tabia” alisema. Ni vigumu kwa mwananchi kuona uhusiano kati ya yeye kusajili kifo cha ndugu yake na maendeleo ya nchi alisema. “Nafahamu zipo nchi ambazo walishaacha kufanya sensa kama tunayofanya kila baada ya miaka kumi na kutumia fedha nyingi kwani nchi hizo wameweka utaratibu ambapo kila mtoto anayezaliwa anasajiliwa na kila mtu anayefariki anasajiliwa hivyo wanakuwa na takwimu za wananchi wake kila siku” alisema Masenza.

Katika kufanikisha zoezi hili, uhamasishaji wa hali ya juu unahitajika alisema mkuu wa Mkoa. Aidha, aliwataka wajumbe wote kuhakikisha ujumbe sahihi unawafikia wananchi ambao wanahitajika kubadili fikra na kuanza kuwa na mtazamo chanya katika usajili wa matukio ya vifo, alisema.

Majaribio ya maboresho ya mfumo wa usajili wa vifo yanafanyika kwa mara ya kwanza katika Mkoa wa Iringa kutokana na mkoa huo kufanya vizuri katika zoezi la usajili watoto wenye umri chini ya miaka mitano na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa.

=30=


Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 17, 2022
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KONGAMANO LA FUNDI SMART LAFANYIKA LEO IRINGA .

    March 17, 2023
  • Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima O. Dendego akifungua kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo tarehe 25/03/2023 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya İringa

    March 14, 2023
  • TUNATAKA KUONA MAPINDUZI YA KIJANI KATIKA MKOA WA IRINGA: RC DENDEGO

    February 28, 2023
  • FANYENI KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    February 21, 2023
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA ZAHANATI YA ITAGUTWA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2021, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.