• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC HAPI KUJENGA KITUO CHA SAYANSI NA TEKNOLOJIA IRINGA

Posted on: October 17th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, IRINGA

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi kujenga kituo cha kuibua vipaji vya sayansi na teknolojia ili kuibua na kuchochea ubunifu kwa vijana mkoani hapa.

Kauli hiyo aliitoa katika hafla fupi ya kupokea na kukabidhi kompyuta 20 ambazo ni ufadhili wa mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa, Mhe Rita Kabati katika ukumbi wa shule ya sekondari Lugalo leo.

Mhe Hapi alisema “nafikiria kuanzisha kituo cha kuibua na kukuza vipaji vya sayansi, teknolojia na ubunifu kwa vijana katika Mkoa wa Iringa. Kituo hiki nataka kiwe na kompyuta za kutosha na mtandao wa intaneti wa bure ili vijana waje wabuni mawazo yao na kuyaendeleza katika kituo hicho”. Alisema kuwa katika kituo hicho, shirika la kuhudumia viwanda vidogo, mamlaka ya mawasiliano Tanzania na wadau wengine wanaohusika na uibuaji na ukuzaji wa sayansi na teknolojia watashirikishwa.

Mkuu wa Mkoa aliahidi kuendelea kuwaunga mkono wale wote wenye nia ya kuleta maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Iringa. “Ndugu zangu, tusikate tama, tusonge mbele katika kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo” alisisitiza Mhe Hapi.

Wakati huohuo, Mbunge wa viti maalum, Mkoa wa Iringa, Mhe Rita Kabati, aliishukuru Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kudhamini shindano la masomo ya sayansi kwa shule za sekondari Mkoa wa Iringa zinazofundisha masomo ya sayansi. Alisema kuwa nchi inapoelekea katika uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025, lazima vijana waandaliwe katika masomo ya sayansi na ufundi. Aliongelea changamoto ya upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi na maabara katika Mkoa wa Iringa kuwa ni jambo linalohitaji nguvu ya pamoja.

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa amewezesha upatikanaji wa kompyuta 20, kati ya hizo, 11 kwa ajili ya Manispaa ya Iringa na tisa kwa ajili ya shule za Halmashauri za wilaya za Mkoa wa Iringa.

=30=  




Matangazo

  • MAADHIMISHO YA UTALII KARIBU KUSINI 2023 May 01, 2023
  • MAADHIMISHO YA KARIBU KUSINI MWAKA 2022 September 19, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAJIPANGA KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI NA WATOTO WACHANGA

    September 14, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWATAKA WANANCHI KUACHANA NA MAFUNDISHO POTOFU

    September 10, 2023
  • MAONESHO YA KIMATAIFA UTALII KARIBU KUSINI 2023

    September 07, 2023
  • PONGEZI

    August 25, 2023
  • Tazama zote

Video

WANANCHI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA UWEPO WA MAONYESHO YA KARIBU KUSINI 2023
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2023, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.