• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Makamu wa Rais Kuanza Ziara ya Siku Tano Mkoani Iringa

Posted on: February 8th, 2018

Anaandika Atley Kuni- TAMISEMI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuanza ziara ya Kikazi kwa muda wa Siku tano Mkoani Iringa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenda kwa vyombo vya  habari na Mkuu wa mkoa wa Iringa Mh. Amina Masenza, imesema ziara hiyo pamoja na mambo mengine vilevile, Makamu wa Rais atapata fursa yakuongea na kusalimiana na wananchi wa mkoa huo

Masenza amesema, Mapokezi ya Mheshimiwa Makamu wa Rais yatafanyika kwenye Kijiji cha Kising’a Wilaya ya Iringa majira ya saa 3.45 asubuhi.

Ndugu zangu mara baada ya mapokezi  Makamu wa Rais atafungua wodi ya Kissing’a lakini pia atakagua upanuzi wa kiwanda cha IVORY, sambamba na kukagua kiwanda cha ufungashaji mazao ya Mbogamboga na Jioni ya siku hiyo hiyo atapokea  taarifa ya Mkoa na kuzungumza na viongozi wa taasisi mbali mbali mkoani humo.

Mheshimiwa Masenza amefafanua kuwa katika siku yake ya pili Mheshimiwa  Makamu wa Rais ataelekea Wilaya ya kilolo ambapo atazindua jengo la utawala shule ya Sekondari kilolo na atafanya mkutano wa Hadhara katika eneo la Ilula.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Mkuu wa Mkoa na kusambazwa katika vyombo vya habari imeonesha siku tarehe 11Februari 2018 Mhe. Makamu wa Rais ataweka jiwe la msingi katika maabara kwenye shule ya Sekondari Mgololo na atafungua zahanati ya Kijiji cha Mtili na kukagua kiwanda cha utengenezaji Mkaa Mafinga.

Masenza alifafanua kwamba katika siku zote hizo  Mheshimiwa Makamu wa Rais atapata pia fursa ya kuzindua mradi wa kuendeleza utalii ukanda wa kusini (REGROW) ambapo Mkoa wa Iringa ni kitovu cha Utalii utakaofanyika kwenye  eneo la kihesa kilolo kuanzia majira ya saa 3:00 asubuhi na majira ya saa  8:00 Mchana atafanya Mkutano wa Hadhara Mwembetogwa katika Manispaa ya Iringa.

Hata hivyo Mh. Masenza amefafanua kuwa, siku ya tarehe 13 Januari, 2018 atafanya majumuisho kabla yakuondoka mkoani humo.

Mh. Masenza amewaomba wananchi wa Iringa kujitokeza kwa wingi ili kumlaki kiongozi huyo wa Kitaifa.

“Natoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi na kwa shamrashamra, nderemo na vifijo na furaha tele wakati wa mapokezi na maeneo yote ya miradi anayotembelea ambapo atapata fursa ya kuwasalimia wananchi” amenukuliwa Masenza.

=30=


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC SERUKAMBA AMESHIRIKI NA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MAZISHI YA MDOGO WAKE NA WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU MHE WILLIAM LUKUVI

    June 07, 2025
  • WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA

    June 06, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA KITAIFA YATAFANYIKA MKOA WA IRINGA

    June 02, 2025
  • KAMBI YA MADAKTARI BINGWA YA MAMA SAMIA YATUA IRINGA

    June 02, 2025
  • Tazama zote

Video

WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.