• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MAANDAMANO YA AMANI

Posted on: June 24th, 2017

MKOA WA IRINGA WAFANYA MAANDAMANO YA KUMPONGEZA JPM

 Na. Mwandishi Maalum, Iringa

Wananchi wa mkoa wa Iringa wamefanya maandamano makubwa ya amani ya kumpongeza Rais Dk John Magufuli kwa kuimarisha uchumi na kulinda rasilimali za Taifa.

Katika maelezo ya maandamano ya amani ya wananchi wa mkoa wa Iringa yaliyotolewa na mratibu wa maandamano hayo, Paschal Mhongole katika uwanja wa Mwembetogwa  leo asubuhi alisema kuwa wananchi wameamua kuandamana ili kumuonesha Rais Dk Magufuli kuwa wanamuunga mkono katika kuimarisha uchumi na kulinda rasilimali za Tanzania.

Mhongole alisema kuwa baada ya Rais Dk Magufuli kupokea taarifa mbili za kamati za kuchunguza makinikia, yalianza kutolewa maombi kutoka kwa wananchi na makundi mbalimbali juu ya umuhimu wa kufanya maandamano ya amani ya kumuunga mkono Rais Dk Magufuli. “Hivyo wazee waliamua kwenda kumuona mkuu wa mkoa ili kumuomba wananchi kufanya maandamano hayo” alisema Mhongole.

Katika salamu za mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema “katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020, inasema kuwa CCM itazielekeza serikali zake kuondoa umasikini, kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa na kusimamia amani, ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao”. Alitoa wito kwa wananchi wote kuungana pamoja kumuunga mkono Rais Dk Magufuli ili Mungu aendelee kumlinda na kumpa nguvu na ujasili katika mapambano yake ya kuwakomboa wanyonge wa Tanzania.

Aidha, aliwataka wananchi kufanya kazi kwa bidii. “Kwa wale walio katika ofisi timizeni wajibu wenu. Kwa wale mlio katika sekta binafsi timizeni wajibu wenu ili wote kwa pamoja tukuze uchumi na kuzalisha malighafi zitakazotumika katika viwanda” alisisitiza Masenza.

Katika maoni ya Maria Sangana, mkazi wa Manispaa ya Iringa kuhusiana na utendaji kazi wa Rais Dk Magufuli, alisema kuwa Rais Dk Magufuli ni mchapa kazi hodari na ni chachu kwa watumishi wengine na wananchi kwa ujumla kuinga utendaji wake ili kukuza uchumi wa Tanzania. “Hata ukiangalia tu muitikio wa wananchi katika maandamano haya ni mzuri. Hii inaashiria kuwa wananchi wengi wanamuunga mkono Rais wetu. Hata ukiangalia ujumbe ulioandikwa katika mabango unasadifu imani waadamanaji waliyonayo kwa Rais” alisisitiza Sangana.

=30=



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC SERUKAMBA AMESHIRIKI NA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MAZISHI YA MDOGO WAKE NA WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU MHE WILLIAM LUKUVI

    June 07, 2025
  • WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA

    June 06, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA KITAIFA YATAFANYIKA MKOA WA IRINGA

    June 02, 2025
  • KAMBI YA MADAKTARI BINGWA YA MAMA SAMIA YATUA IRINGA

    June 02, 2025
  • Tazama zote

Video

WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.