• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

IRINGA YAKAGUA YA MIRADI 18 KUJIRIDHISHA NA THAMANI YA FEDHA- RC MASENZA

Posted on: May 23rd, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa umekagua miradi 18 ya maendeleo yenye zaidi ya shilingi bilioni tatu katika sekta mbalimbali ili kijiridhisha na thamani ya fedha katika utekelezaji wa dhana ya utawala bora.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akisoma taarifa ya mkoa wa Iringa wakati wa kupokea Mwenge wa uhuru kutoka Mkoa wa Mbeya leo.

Masenza alisema kuwa Mkoa kupitia taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) imekagua miradi 18 ya maendeleo katika sekta za maji, elimu na barabara. Miradi hiyo ilikuwa na thamani ya shilingi 3,380,725,980.72. Alisema kuwa lengo la ukaguzi huo ni kufuatilia matumizi na thamani ya fedha katika miradi hiyo. Zimefanyika kazi 12 katika kudhibiti mianya ya rushwa kwa kuchambua mifumo sita na kufanya warsha sita na wadau wa mapambano ya rushwa alisema Masenza.

Katika hatua nyingine, TAKUKURU Mkoa wa Iringa imetoa elimu ya mapambano dhidi ya rushwa na madhara yake kwa wananchi 4,909 kupitia semina 52, mikutano ya hadhara 25, klabu za wapinga rushwa 63. Aidha, machapisho 1,259 yenye ujumbe wa mapambano dhidi ya rushwa yamegawiwa kwa wananchi.

Akiongelea watuhumiwa wa makossa ya rushwa waliofikishwa mahakamani, mkuu wa Mkoa alisema kuwa watuhumiwa wa makosa ya rushwa kwa kesi nne na majalada 13 ya uchunguzi yakikamilika baada ya kupokea malalamiko 126 ya rushwa. Uchunguzi wa malalamiko mengine unaendelea alisema.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa mapambano dhidi ya rushwa yatawezekana ikiwa kaulimbiu ya mapambano hayo isemayo ‘kataa rushwa-jenga tanzania’ itatekelezwa kwa vitendo.

Mwenge wa uhuru mkoani Iringa utakimbizwa katika Wilaya tatu  na halmashauri tano ukikagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi 40 ya maendeleo.

=30=



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.