• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

IRINGA NAFASI YA NNE KITAIFA MTIHANI DARASA LA SABA

Posted on: June 8th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa umeshika nafasi ya nne kitaifa katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2017 kati ya mikoa 26 ya Tanzania bara.

Kauli hiyo ilitolewa na kaimu afisa elimu Mkoa wa Iringa, Mwl Farida Mwasumilwe alipokuwa akisoma taarifa ya maadhimisho ya wiki ya kusoma mkoani Iringa yaliyofanyika katika mji mdogo wa Ilula wilayani Kilolo.

Mwl Mwasumilwe alisema kuwa Mkoa wa Iringa ni miongoni mwa mikoa inayofanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba. “Kwa mtihani uliofanyika mwezi Septemba, 2017 Mkoa umeshika nafasi ya 4 kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara ukiwa na ufaulu wa asilimia 83.14 ambapo jumla ya wanafunzi 20,606 wamechaguliwa na kujiunga na kidato cha kwanza 2018. Aliongeza kuwa ufaulu wa mwaka 2015 Mkoa ulikuwa nafasi ya 10 ukiwa na ufaulu wa asilimia 73.25. Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Wilaya ya Kilolo ufaulu umekuwa ukiongezeka kuanzia mwaka 2015-2017” alisema Mwl Mwasumilwe.

Akiongelea shule 10 zilizofanya vizuri ngazi ya Mkoa, Mwl Mwasumilwe alisema kuwa Mkoa ulikuwa na shule 481 zilizofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi.

Katika shule 10 zilizofanya vizuri kimkoa, shule tatu ni za serikali na saba ni binafsi, alisema. Alizitaja shule hizo kuwa ni Sipto (Manispaa), St Dominic Savio (Manispaa), Star (Manispaa), Ukombozi (Manispaa), BrookeBond (Mufindi), Ummusalama (Manispaa), Lukwambe (Iringa DC), St Charles (Manispaa), Southern Highlands (Mji Mafinga) na Nyamalala (Mji Mafinga)

Maadhimisho ya wiki ya kusoma mkoani Iringa yaliongozwa na kaulimbiu isemayo “Stadi za kusoma, kuandika, na kuhesabu ni msingi wa elimu; tuwekeze katika elimu kuelekea uchumi wa viwanda”.

=30=


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.