THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA - PRIME MINISTERS OFFICE
   
Search the site

 
 .: Home
 .: Organization structure
 .: About Us & Contact
 .: Mission & Vision
 .: Project & Programs
 .: Financial Report & Budget
 .: Documents
Taarifa za idara

 .: Kilimo na Mifugo

.: Maliasili

.: Elimu

.: Afya

.: Maji

.: Ushirika

.: Biashara

.: Barabara na Majengo

.: Ardhi, Upimaji na Ramani

.: Jamii, Jinsia & Watoto

 

Huduma za kiuchumi

Mkoa wa Iringa una jumla ya eneo la hekta 58,936,000 kati ya hizo km za mraba 56,864 ni nchi kavu na km za mraba 2,072 ni eneo la maji. Kati ya eneo lote hekta 43,935,000 (74%) linafaa kwa kilimo, ingawa hadi sasa hekta zinazotumika kwa kilimo ni 7,468,950 tu sawa na asilimia 17. Mazao makuu ya biashara na chakula ambayo yanalimwa ni pamoja na Mahindi, Ngano, Pareto, Chai, Viazi mviringo, Matunda, Alizeti, Karanga, Ufuta, Maharage, Nyanya, Mpunga, Tumbaku, Soya, Mtama, Mhogo, Korosho, Artemisia na Paprika.

Eneo linalilimwa mazao mbalimbali limeongezeka kutoka hekta 586,245 mwaka 2005/2006 hadi kufikia hekta 746,895 zilizolimwa msimu wa 2007/2008.Elimu ya kilmo bora ilitolewa kwa wakulima na jumla ya mashamba darasa 750 yalizalishwa na jumla ya wakulima 18,750 wamepatiwa mafunzo kwa vitendo kupitia mashamba haya kwa kipindi cha Desemba 2005 hadi Desemba 2008. Mbolea na nbegu zilizotumika mwaka 2005/2006 zilikuwa tani 12,121 na tani 833 kwa pamoja. Ukilinganisha na tani 45,260 za mbolea na tani 1,125 za mbegu mwaka 2008hii ni sawa na asilimia 53 kwa matumizi ya mbolea na asilimia 26 kwa matumizi ya mbegu.

Uzalishaji wa Mazao makuu ya chakulu na biashara mwaka 2005/2006hadi 2007/2008

Mazao 2005/2006 2006/2007 2007/2008
Hekta limwa Mavuno (Tani) Hekta limwa Mavuno (Tani) Hekta limwa Mavuno (Tani)
Mahindi 305,877 429,106 378,520 641,854 384,509 739,370
Maharage 56,767 49,327 73,839 58,551 68,772 83,001
V/Mviringo 33,750 286,289 37,194 287,973 33,177 298,455
V/Vitamu 4,978 35,288 10,409 34,051 8,569 31,976
Mpunga 7,238 13,842 13,538 32,001 16,693 36,032
Ngano 10,2195,665 11,155 17,719 21,165 19,515 21,196
Njegere 5,665 9,216 11,300 11,413 6,187 22,817
Kunde 13,079 13,588 15,009 35,053 24,710 38,936
Karanga 3,421 2,860 4,908 5,940 8,753 12,202
Ulezi 1,308 1,109 1,276 1,453 1,662 1,941
Jumla 442,302 851,780 563,712 1,129,454 572,547 1,285,926

Mifugo

Mkoa una jumla ya mifugo ya Mashamba ya mifugo 12 yanayomilikiwa na Serikali na watu binafsi. Mashamba haya huzalisha Maziwa, Mitamba na Madume. Madume haya hutumiwa zaidi na wakulima wadogo kuboresha mifugo yao.

Takwimu za sekta ya Mifugo Mifugo kwa kipindi cha Desemba 2005 hadi Desemba 2008

Takwimu / Huduma Desemba 2005 Desemba 2008 Ongezeko / Mafanikio
Idadi ya Ng'ombe wa kienyeji 559,597 420,187 Idadi ya Ng'ombe imepungua kwa 24% baada ya wafugaji kuzingatia wa kibiashara na ubora wake na sio wingi wake.
Idadi ya Ng'ombe wa maziwa na nyama (kisasa) 20,289 28,020 Idadi imeongezeka kwa 38%
Miundo mbinu Majosho yaliyokuwepo - 226, yalikarabatiwa - 72 na yaliyotumika 88 Majosho yaliyopo - 229, yaliyokarabatiwa - 93 na yaliyotumika 161. Majosho yanayofanya kazi yameongezeka yadi kufikia 161 sawa na 82.9% ongezeko hili kubwa ni baada ya selikari kusambaza dawa ya ruzuku.
Uzalishaji wa maziwa na nyama Maziwa lt 4,592,662, Nyama jumla ya mifugo (n'gombe, kondoo, mbuzi na nguruwe) 62,102walichinjwa N'gombe 26,568 kondoo/mbuzi17,970 na nguruwe 17,564 Mazwa lt 6,976,018 Nyama jumla ya mifugo, ( N'gombe, kondoo, mbuza na nguruwe) 72,634 walichinjwa, Ngombe 26,379, kondoo/mbuzi 22,008 na nguruwe 24,247 Lita 2,383,356 ikiwa ni ongezeko la 52%
Uogeshaji Idadi ya miruko ng'ombe 802,220, Mbuzi 107,133, Kondoo 71,372 na Mbwa 10,728. Idadi ya miruko Ng;ombe 1,513,056, Mbuzi 404,024, Kondoo 135,121 na Mbwa 26,728 Ongezeko la miruko kwa ng;ombe ni 88.6%
Zao ngozi vipande 16,568 vya ngozi ya ng'ombeviliuzwa. vipande 13,970 vya ngozi ya kondoo/mbuzi viliuzwa Vipande 18,375 vya ngozi ya ng'ombe viliuzwa. Vipande 17,970 vya ngozi ya kondoo/mbuzi viliuzwa.

Uboreshaji wa ufugaji wa kuku wa kisasa na kienyeji

Chanjo ya mdondo - kuku waliochanjwa ni 200,000 kuku waliochanjwa kuzuia mdondo ni 1,257,413 Ongezeko ni kuku 1,057, 413 sawa na 528.7% hii ni kwa sababu ya matumizi ya dawa ya matone ya i2 sanjari na kampeni ya chanjo kwa kuku wa kienyeji.

 

opyright © 2009 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, P.O.BOX 858, Iringa, TEL: 026 - 2702715, FAX: 026-2702082 / 2701888

[Go Home]