THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA - PRIME MINISTERS OFFICE
   
Search the site

 
 .: Home
 .: Organization structure
 .: About Us & Contact
 .: Mission & Vision
 .: Project & Programs
 .: Financial Report & Budget
 .: Documents
Taarifa za idara

 .: Kilimo na Mifugo

.: Maliasili

.: Elimu

.: Afya

.: Maji

.: Ushirika

.: Biashara

.: Barabara na Majengo

.: Ardhi, Upimaji na Ramani

.: Jamii, Jinsia & Watoto

Ardhi

Katika utekelezaji wa Sera ya Ardhi ya mwaka 1995 na Ilani ya uchaguzi - ibara ya 42 Mkoa umeweza kufanya wafuatayo kati ya Desemba 2005 hadi Desemba 2008:

  • Kukamilisha upimaji wa vijiji 411 hivyo kufanya idadi ya vijiji kuwa 703 vilivyostahili kupimwa Mkoani.
  • Kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji 88.
  • Sheria ya ardhi No. 5 ya vijiji imetolewa kwa vijiji 338, vyeti vya ardhi 157 vimeandaliwa na hati miliki kamili 980 zimeandaliwa.
  • Jumla ya viwanja 6,085 vimepimwa katika miji ya Makambako, Mafinga, Kitongoji cha Tungamalenga, Mji wa Njombe na Manispaa ya Iringa. Ambako hati miliki kisheria 1,484zimeandaliwa.
  • Maandiko ya mkopo kwa Halmashauri ya Wiliya ya Iringa, Manispaa yamewasiliashwa Wizara ya Ardhi.
  • Mkoa umeweza kuanzisha mfuko wa kuendeleza upimaji wa viwanja, na kuweza kuikopesha Manispaa ya Iringa Tsh 29,000,000/=. Aidha, Wizara ya Ardhi imeweza kuikopesha Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Tsh 30,000,000/= na Mamlaka ya Mji Mdogo wa Makambako Tsh 40,000,000/= kwa ajiri ya upimaji na uendelezaji ardhi.

Sekta ya Mipango Miji

  • Imeweza kuainisha maeneo yaliyojengwa kiholela katika Manispaa ya Iringa mjini, Mji Njombe, Miji midogo ya Ilula na Makambako.
  • Kuandaa mipango ya kina kwa maeneo mapya (Detailed Planning Schems for New Areas) kwa vitongoji vya Kidamali, Tungamalenga (Halmashauri ya Iringa) na Ilembula Halmashauri Wilaya ya Njombe.
  • Kusimamia uendelezaji wa maeneo ya kati ya mji (CDB) kwa maeneo ya Miyomboni, Stand kuu na Wilolesi (RETCO) katika Manispaa ya Iringa.
  • Kutayarisha michoro ya mipango miji 44 yenye jumla ya viwanja 12,911 katika miji ya Njombe, Mafinga, Makambako, Kidamali, Tungamalenga, Kilolo, Ilula na Manspaa ya Iringa.

 

opyright © 2009 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, P.O.BOX 858, Iringa, TEL: 026 - 2702715, FAX: 026-2702082 / 2701888

[Go Home]