|
|
Ardhi
Katika utekelezaji wa Sera ya Ardhi ya mwaka 1995 na Ilani ya uchaguzi - ibara ya 42 Mkoa umeweza kufanya wafuatayo kati ya Desemba 2005 hadi Desemba 2008:
- Kukamilisha upimaji wa vijiji 411 hivyo kufanya idadi ya vijiji kuwa 703 vilivyostahili kupimwa Mkoani.
- Kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji 88.
- Sheria ya ardhi No. 5 ya vijiji imetolewa kwa vijiji 338, vyeti vya ardhi 157 vimeandaliwa na hati miliki kamili 980 zimeandaliwa.
- Jumla ya viwanja 6,085 vimepimwa katika miji ya Makambako, Mafinga, Kitongoji cha Tungamalenga, Mji wa Njombe na Manispaa ya Iringa. Ambako hati miliki kisheria 1,484zimeandaliwa.
- Maandiko ya mkopo kwa Halmashauri ya Wiliya ya Iringa, Manispaa yamewasiliashwa Wizara ya Ardhi.
- Mkoa umeweza kuanzisha mfuko wa kuendeleza upimaji wa viwanja, na kuweza kuikopesha Manispaa ya Iringa Tsh 29,000,000/=. Aidha, Wizara ya Ardhi imeweza kuikopesha Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Tsh 30,000,000/= na Mamlaka ya Mji Mdogo wa Makambako Tsh 40,000,000/= kwa ajiri ya upimaji na uendelezaji ardhi.
Sekta ya Mipango Miji
- Imeweza kuainisha maeneo yaliyojengwa kiholela katika Manispaa ya Iringa mjini, Mji Njombe, Miji midogo ya Ilula na Makambako.
- Kuandaa mipango ya kina kwa maeneo mapya (Detailed Planning Schems for New Areas) kwa vitongoji vya Kidamali, Tungamalenga (Halmashauri ya Iringa) na Ilembula Halmashauri Wilaya ya Njombe.
- Kusimamia uendelezaji wa maeneo ya kati ya mji (CDB) kwa maeneo ya Miyomboni, Stand kuu na Wilolesi (RETCO) katika Manispaa ya Iringa.
- Kutayarisha michoro ya mipango miji 44 yenye jumla ya viwanja 12,911 katika miji ya Njombe, Mafinga, Makambako, Kidamali, Tungamalenga, Kilolo, Ilula na Manspaa ya Iringa.
|