|
|
Ardhi
Katika utekelezaji wa Sera ya Ardhi ya mwaka 1995 na ilani ya uchaguzi - ibara ya 42 mkoa umeweza kufanya wafuatayo kati ya desemba 2005 hadi Desemba 2008:
- Kukamilisha upimaji wa vijiji 411 hivyo kufanya idadi ya vijiji kuwa 703 vilivyostahili kupima Mkoani.
- Kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji 88.
- Sheria ya ardhi no 5 ya vijiji imetolewa kwa vijiji 338, vyeti vya ardhi 157 vimeandaliwa na hati miliki kamili 980 zimeandaliwa.
- Jumla ya viwanja 6,085 vimepimwa katika miji ya Makambako, Mafinga, Kitongoji cha Tungamalenga, Mji wa Njombe na Manispaa ya Iringa. Ambako hati miliki kisheria 1,484zimeandaliwa.
- Maandiko ya mkopo kwa Halmashauli ya Wiliya Iringa,manispaa yamewasiliasha Wiwara ya Ardhi.
- Mkoa umeweza kuanzisha mfuko wa kuendeleza upimaji wa viwanja, na kuweza kuikopesha manispaa ya airinga Tsh 29,000,000/=. Aidha, wizara ya Ardhi imeweza kukopesha Halmashauli ya Wilaya ya Kilolo Tsh 30,000,000/= na Mamlaka ya mji Mdogo wa Makambako Tsh 40,000,000/= kwa ajiri ya upimaji na uwendelezaji ardhi.
Sekta ya Mipango Miji
- Imeweza kuainisha maeneo yaliyojengwa kiholela katika Manspaa ya Iringa mjini, Mji njombe, miji midogo ya Ilula na Makambako.
- Kuandaa mipango ya kina kwa maeneo mapya (Detailed Planning Schems for New Areas) kwa vitongoji vya Kidamali, Tungamalenga (Halmashauri ya Iringa) na Ilembula Halmashauri Wilaya ya Njombe.
- Kusimamia uendelezaji wa maeneo ya kati ya mji (CDB) kwa maeneo ya Miyomboni, Stand kuu na Wilolesi (ERTCO) katika Manispaa ya Iringa.
- Kutaarisha michoro ya mipango miji 44 yenye jumla ya viwanja 12,911 katika miji ya Njombe, Mafinga, Makambako, Kidamali, Tungamalenga, Kilolo, Ilula na Manspaa ya Iringa.
|